Translate

Friday, May 28, 2010

BANK ZA SHARIA ZA KIISLAMU: MWANZO WA KUTEKWA NA UCHUMI WA KIISLAMU?

Taarifa za kuanzishwa Benki zinazofuata mfumo wa sharia yaani wa kutotoza riba kwa fedha zitakazowekwa katika benki hizo zimezua hofu miongoni wa wafuasi wa imani zingine wakijihoji kuwa je huu ndiyo mwanzo wa uchumi wa Tanzania kutawaliwa na uchumi wa Kiislamu? Changamoto kwa Knisa la Tanzania kuendelea kuanzisha Benki nyingi zinazomilikiwa na Makanisa kuliko zilizopo sasa ili kukabiliana na ushindani utakaokuwepo. Je Jihad ya Benki hizo itahusisha harakati za kutaka kuisilimisha Tanzania kama baadhi ya Viongozi wa Tanzania walio Waislamu wanavyotaka tujiunge na Umoja wa Hadhara ya Kiislamu duniani yaani, OIC? Kanisa kwa hili tusibweteke yasije yakatukuta kama yaliyo wakuta nchi za wenzetu waliokuwa wanapuuza harakati kama hizi na matokeo yake leo wamemezwa kabisa ikiwemo kuminywa uhuru wao wa kuabudu na nchi hizo kutajwa kuwa ni za mfumo wa Kiislamu. Mbinu ni nyingi tuanze na hii.

1 comments:

Anonymous said...

Kaka Dan.asante kwa umakini wako katika kufuatilia mambo yanayohusu imani pamoja na nchi yetu nzuri-Tanzania.

Jambo moja linanishangaza kwa kanisa la Tanzania ni kwamba haliwezi kuona tatizo right at the begining na kuchukua hatua mathubuti za kupambana, bali utaona viongozi wa kanisa wanaamka baada ya mambo kuota mizizi. Well, Mungu atalipigania kanisa lake lakini "where is the church's prophetic voice?" Mi nadhani iko haja ya kuwa-confront viongozi wetu wa Kiimani waamke!!

 
Powered by Blogger